UISLAMU NA DEMOKRASI

April 28, 2008 / by www.maduru

BISMILLAHIR RHMAANIR RHYIM 

 

ENYI WASLAMU JIFUNGENI NA  HUKMU ZA KISHERIA WALA  MUSISHIRIKI  KATIKA KURA CHINI YA NIDHAMU YA KIILMANIYYA KIDEMOKRASIA ILIOBUNIWA JUU YA UKAFIRI

 

 Mwezi Disemba 2007 kunatarajiwa kutokea uchaguzi mkuu wa kumi, na tayari  wimbo wa demokrasia wa vyama vingi wasikika kote nchini, wakati huo huo badhi ya waislamu na makundi yao yanayodai kuzungumza   kwa niaba ya waislamu wamewaunga mkono wagombeaji fulani na vyama vyao, hata kama  wagombeaji hao si waislamu kuzidisha mambo utata baadhi yao wanahamasisha waislam kufikia kiwango cha kudai kuwa eti kupiga kura ni jihadi na ni wajibu wa kidini. Ni muhimu kwa waislamu  wacha mungu kutambua hali halisi ya kidemokrasia ya vyama vingi kabla kuambatanisha na dalili za kisheria  zilizowazi, na kwa mujibu wake wajifunge na hukmu za kisheria bila ya kujali maslahi yake ya kibinafsi.  

Demokrasia ni nidhamu     ya kiutawala ya kimagharibi iliyobuniwa juu ya itikadi ya Kiilmaniyya, Mayunani wa zama za kale ndio wa mwanzo waliozua agenda hiyo kasha baadaye ikahusishwa upya katika mapinduzi yaliyotokea ufaransa mwaka 1789 na kunukuliwa katika    katiba ya Amerika mwaka 1776. Ilmaniyya humaanisha binadamu atenganishe dini yake na maisha yake, na dini ibakie kuwa ibada chache zinazofungika katika majumba ya ibada bila ya kuwa na usemi wowote au muongozo kwa yale yanayojili nje ya majumba ya ibada. Ilmaniyya [secularism] latokana na tamko la `kiyanuni` Linalomaanisha kilichoko nje ya hekalu [jumba la ibada ]mfano mambo yanayohusu mahusiano baina ya mke na mume, katiba, ukadhi, uchumi n,k ambapo mtu hupewa ruhusa ya kuendesha maisha yake kwa matamanio yake kwa mujibu ya kanuni zilizotungwa na wanadamu bila ya kujali muongozo wa kidini, akhlaqi au mila.

Kwa hivyo sheria ya muumba hufungwa ndani ya majumba ya ibada, huku mwanadamu akijitweka ubwana wa yale yaliyo nje yake. Demokrasia linatokamana na matamko mawili ya kiyunani [demos kratos] kwa maana utawala kwa watu ambao maana yake ni watu wanamiliki ubwana kamili na uhuru usiokuwa na vikwazo wa kutunga sheria  ili kupeleka maisha yao, kazi ambayo haimstahiki ila muumba. Ndio utayaona mabunge yote ulimwenguni yakihalalisha yale aliyoyaharamisha allah kwa njia ya kukatikiwa kama kumtukana mtume [saw] kamari, tiba,  zinaa, tembo, kumtawaza kafiri kama mtawala wa waislamu n,k na wakati huo huo huharamisha yale aliyoyafaradhisha  Allah kwa njia ya kukatikiwa kama kuvaa hijab, kulingania umoja wa ummah chini ya serikali ya khilafah, kupigana jihad n.k.

Enyi waislamu dalili za kisheria ziko wazi katika kukufurisha itikadi ya kiilmaniyya na matunda yake ya demokrasia na uhuru n,k. aqeeda ya kiislamu imedhihirisha wazi kuwa ubwana ni wa allah [swt] peke yake bila ya kushirikishwa na  yeyote na sheria yake ndio yenye kutawala nyanja zote maishani, sawa sawa ndani ya msikiti au nje yake, Asema Ta`ala:

 Hakuna hukumu  ila ya Allah(tu) (Yusufu:40)  Na asema Taala: Naapa kwa mola wako miezi hawajaamini [kikweli ] mpaka wakufanya [wewe ndiye ] hakimu katika yale wanayo khitalafiana, kasha wasione uzito nyoyoni juu ya hukmu uliyoitoa na wanyenyekee kikamilifu [tmq  4: 63]

Haifai kata kata kwa muislamu yeyote kukubali mwito wa kikafiri wa ki ilmaniyya na nidhamu ya kidemokrasia inayomruhusu mwanadamu kutunga sheria na kupuuza sheria ya Allah Asemaa Ta`ala                                            Haiwi kwa muumini wa kiume wala wa kike pindi Allah na mtume wake wanapo kata shauri wawe na hiari katika shauri [tmq  al ahzaab

36]  Allah [swt] ameteremsha dini kamili ya kiislamu yenye hukmu katika kila nyanja ya maisha iwe katika ibaadat,uchumi,siasa,katiba akhlaqi n,k ili kumuongoza muislam katika mambo yake yote na sheria ya kiislam pasina kuwa na khiyari ya kutunga sheria zake mwenyewe Asema ta`alah: 

 Na tumekutelemshia kitabu kielezacho kila kitu na Asema taalah:

 Leo nimekukamilishieni Dini yenu  na kukutimizieni neema yangu, na nimeridhika uislam kuwa ndio dini yenu pekee(Almaidah) Kafiri pekee ndiye anayeweza kuchagua hukmu ya kidhulma na kijahiyya zilizotungwa na wanadamu haya ya sheria ya allah [swt] anasema ta`ala                      

Hao wanataka hukmu za kijahiliyya na ni nani aliye mwema zaidi katika hukmu kuliko allah [yanayofahamika haya] na watu wenye yakini [tmq al maidah 50] anasema ta`ala:                               

 uwaoni wale wanaodai kwamba wanaamini yale yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyotelemshwa kabla yake?  na wanataka kuhukumiwa kwa twaghuti [njia isiyowafiki sheria]hali wameamrishwa kukana twaghuti [tmq  an nisaa 60] 

Enyi waislamu tahadharini nakila mwenye kuwalingania, aidha kimakusudi au kwa kutojua, kushiriki katika uchaguzi kwenye nidhamu ya ki ilmaniyya ya kidemokrasia kwani huyo anawalingania kwenye ukafiri. Juu ya hayo yawalingania musimame pamoja namaadui zetu  wamagharibi wa wa-koloni wa ki-misalaba wakiongozwa na Amerika wanaopiga vita biladi za kiislamu ili kutabikisha  kwa nguvu nidhamu ya ki-ilmaniya ya kidemokrasia mabadiliko kwa mfumo wa kiislamu  na nidhamu yake ya utawala yaani

Al-khilafah  Ar-rashida.

Enyi waislamu jifungeni na aqeedah sahihi ya kiislamu na mwenendo wa bwana mtume [saw] katika kulingania uislamu kama mfumo kamili wa kimaisha bila ya kushawishika kushiriki katika nidhamu ya kikafiri. waislamu wa Kenya lazima wajifunze kutokana na makosa ya ndugu zao huko Algeria, Misri, Palestina na wenginepo   waliojaribu kutabikisha uislamu kupitia kushiriki katika uchaguzi wa ki ilmaniyya wa kidemokrasia iliyowatia katika mtego wa nidhamu uliotaka imma kuwatumia kwa ajili yamaslahi ya ukafiri au kuwakatisha tama. Allah alimtahadhalisha mtume wake [saw] na mitego ya kikafiri huko makka, na tahadhali hiyo yatukusanya nasi mpaka leo pindi aliposema ta`ala                    

 [makafiri ] wanapenda  uwe laini [kwa kushiriki  nidhamu zao ] nao watakuwa lini kwao [tmq   al  qalam:9 ]  Lazima tumuagize Mtume(saw) aliyeishi katika Daar A-kufrn kama tunavyoishi sisi leo,hakusalimu amri bali alifanya bidii ili kubadilisha hali ya kuwalingania ulinganizi wa kimfumo wa kiislamu kama badili wa fisadi na umaskini unaoletwa  na ukafiri,kupitia mvutano wa kifikra  na mapanbano ya kisiasa bila ya kutumia nguvu. Huku akitumia ukweli na dalili za kiislamu zilizohujumu fikra na misingi ya nidhamu za kikafiri kiarabu zama hizo mpaka kufaulu kuusimamisha Uislamu kupitia dola Dola la kiislamu huko  madina.

Ni madai ya urongo kuwa uislamu wasiposhiriki katika uchaguzi watapata madhara makubwa.Bali waislam walishirika chaguzi zote kutoka `uhuru`na kila mara walipata madhara makubwa yaliyosababisha na nidhamu za kifisadi.Isitoshe kuna jamii zisizokuwa za kiislam zinazoishi Kenya pasina uwakilisha wowote serikalini lakini zimeweza kufanikiwa katika kupeleka maisha yao kwa uchache kupata ufanisi hapa duniani.Amma waislamu lengo letu ni kumridhisha mola wetu hata kama tutapata taabu hapa duniani  na ni jukumu letu kuubeba Uislamu kama mfumo badili ya uovu wa demokrasi ulioneza ufisadi,ukabila,ujinga na maradhi katika Afrika.

Ni urongo zaidi  kudai kuwa waislamu wanawajibika kushiriki kwa ajili ya kisingizio cha `dharura`au `uovu ,Huo ni uwongo kwa sababu waislamu wa Maka zama za Mtume (saw) walikuwa wachache kiidadi na katika hali mbaya zaidi  lakini hawakushiriki katika nidhamu za kikafiri pamoja na kudhulumiwa,kuteswa na hata baadhi yao kuuwawa!Bali walihiyari kufa shahidi kuliko kuuza uislamu wao huku wakijitahidi kutetea haki zao katika Daar Al-kufr pamoja na kudumu katika kutekeleza jukumu lao la kimsingi  la kulingania Uislamu kama suluhisho la kudumu.Na kushiriki katika uchaguzi wa ki-ilmaniyya wa ki-demokrasia ni uovu mkubwa zaidi kwani ndio kuhalalisha ukafiri na kuupiga vita uislamu ambao ndio suluhusho pekee.

Enyi waislamu! Hizb ut-Tahrir  Kenya waliwalingania katika mwezi wa huu Ramadhani kuungana nayo katika kujifunga na hukmu za kisheria na kukwepa mtego wa kushiriki katika nidhamu za ki-ilmaniyya ya ki-demokrasia huku tukifanya bidii kulingania Uislamu utakao eneza uadilifu na haki kote duniani pamoja na kukomboa ulimwengu kutokamana na ufisadi na maovu ya ukafiri. Asema Ta`ala:     

Anachokupeni mtume, kichukuweni na anachowakanyeni nacho kiwacheni.Na mcheni Allah kwani Allah ni mkali wa kuadhibu (Qur Al-Hashir:7)       

0 comments on UISLAMU NA DEMOKRASI

Add a comment

To add comments without entering your email and image verification, you must be logged in. Login or Join Blogster

  • Type the words in the box below the image.

Email this blog post to a friend

To email posts to friends, you must be logged in. Login or Join Blogster

Friends

www.maduru currently has no Blogster friends

Add him as a friend and send him a friendly welcome!